Friday, November 13, 2009

Hiki ndio choo cha mbuyu bwana

Hebu tazama ubunifu huu wa Mwafrika - choo safi kabisa (tena inavyoonekana ni cha "kisasa") ndani ya mbuyu. Hapa hakuna haja ya kiyoyozi wala kipasha joto bali necha ndiyo inatawala.

Mbuyu umekuwa ukitumiwa kama makazi na makabila mengi yanayoishi sehemu kame ambako ndiko hasa mmea huu unastawi vizuri mf. Watindiga na Wafulani. Kuweka choo cha kisasa ndaniye ni kupanua tu matumizi yake ya tangu zamani ingawa si ajabu watu wanaotetea mazingira wakadai kwamba kitendo kama hiki cha kuugeuza mbuyu kuwa choo si kitendo cha kujivunia kwani kinahatarisha maisha yake.

No comments:

Post a Comment